![]() |
Mshambuliaji aliyetekeleza mashambulio hayo alitoroka na hajakamatwa hadi kufikia sasa |
Takriban watu 39 wakiwemo wageni 15
wanahofiwa kuuawa katika shambulio la klabu ya burudani mjini Istanbul
Uturuki, kulingana na waziri wa maswala ya ndani nchini humo.
Mtu
aliyekuwa amejihami kwa bunduki aliwafyatulia risasi watu waliokuwa
wakijiburudisha katika mkahawa huo wa Reina saa saba usiku wakati
ambapo watu walikuwa wakisherehekea kuingia kwa mwaka mpya.Muuaji wa watu 39 katika kilabu
ya burudani Uturuki asakwa
Urusi na Marekani zalaani shambulio Uturuki
Waziri huyo Süleyman Soylu ameelezea waliojeruhiwa kuwa 69 .
![]() |
Kulingana na waziri wa maswala ya ndani takriban watu 39 wamefariki huku 69 wakijeruhiwa |
Baadhi yao iliwabidi kujirusha baharini kuepuka msusuru wa risasi zilizokuwa zinafyatulia.
Polisi mmoja ni miongoni mwa waliofariki.
![]() | ||
Mtu huyo aliingia katika klabu hiyo akijifanya kikaragosi kilichovaa mavazi ya Santa Claus na punde kuanza kuwafyatulia risasi kiholela waliokuwepo. |
Source BBC Swahili
0 comments:
Post a Comment