Monday, January 2, 2017

Islamic State lakiri kutekeleza shambulio Istanbul

Kundi la Islamic State limekiri kutekeleza shambulio la kilabu ya usikju mjini Istanbul Kundi la Islamic State limekiri kuhusika na shambulio baya dhidi ya watu waliokuwa wakiukaribisha mwaka mpya wa 2017 katika klabu moja ya usiku mjini Istanbul Uturuki. Katika taarifa, kundi hilo limemtaja muuaji aliyekuwa na bunduki ya rashasha kama shujaa wa kundi hilo. Huku Polisi wa Uturuki wakiendelea kumsaka mshukiwa huyo mkuu aliyetekeleza...

Kiongozi wa Republican ahofia uongozi wa Trump

Todd Whitman ahofia wajukuu zake chini ya uongozi wa Donald Trump Kiongozi mmoja wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa anahofia maisha ya wajukuu wake saba ,chini ya uongozi wa rais mteule wa Marekani Donald Trump. Christine Todd Whitman ,ambaye ndio mkuu wa shirika la kulinda mazingira nchini Marekani amemshtumu Donad Trump kwa kupuu...

Mlipuaji awaua watu 4 Somalia

Mlipuaji mmoja wa kujitolea muhanga amewaua watu 4 nchini Somalia Habari kutoka mji mkuu wa Somalia, zasema kuwa watu wanne wameuwawa na wengine kadhaa wamejeruhiwa baada ya mlipuaji wa kujitoa kufa alipojilipua karibu na uwanja wa ndege mjini Mogadishu. Idara ya Polisi imesema kuwa, mhanga hu...

Mshambuliaji wa Istanbul alifyatua risasi 180

Mshambuliaji wa mkahawa wa Istanbul anaendelea kusakwa Huku polisi wa Uturuki wakiwa katika harakati za kumsaka mtu aliyetekeleza shambulio katika kilabu moja ya burudani huko mjini Istanbul na kuwauwa watu 39, taarifa za kina zimefichuka kuhusu shambulio hilo. Vyombo vya habari vya Uturuki vimeripoti kuwa shambulio hilo lilidumu kwa dakika 7. Kuna ushahidi unaonesha kuwa mshambuliaji alifika eneo hilo akitumia usafiri...

Wanadiplomasia wa Urusi waliofurushwa Marekani waondoka

Rais wa Urusi na mwenzake wa Marekani Barrack Obama Vyombo vya habari vya Urusi vimeripoti kuwa wanadiplomasia 35 wa Urusi waliofurushwa na rais Barack Obama kutoka Marekani wameondoka wakiandamana na familia zao . Urusi ilituma ndege maalum ya kuwarudisha nyumbani. Wanadiplomasia hao waliamuriwa kuondoka Marekani baada ya Urusi kushtumiwa kuwa ilijaribu kuingilia uchaguzi wa hivi majuzi wa Marekani kwa njia ya udukuzi...

Waziri wa mazingira auawa Burundi

Waziri wa mazingira amepigwa risasi na kufariki nchini Burundi Waziri wa mazingira huko Burundi Emmanuel Niyonkuru, amefariki baada ya kupigwa risasi mjini Bujumbura saa chache tu baada ya kuingia mwaka mpya. Police wanasema amepigwa risasi alipokuwa akielekea nyumbani kwake eneo la Rohero . Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza, ameapa kuchukua hatua kali za kisheria kwa atakayepatikana na hatia ya kuhusika katika mauaji...

Sony yamuomba radhi Britney Spears baada ya ''kumuua''

Britney Spears Kampuni ya muziki ya Sony imemuomba radhi mwanamuziki nyota wa pop Britney Spears, baada ya ukurasa wake rasmi kutangaza kuwa amefariki. Kampuni hiyo ya burudani iliondoa mara moja ujumbe wake batili, ikisema kuwa akaunti yake ilikuwa "imedukuliwa" lakini kwamba hali hiyo "imerekebishwa. Sony iliongeza kusema kuwa '' samahani kwa Britney Spears na mashabiki wake kwa mkanganyiko wowote uliojitokeza". Britney ...

Rubani apatikana mlevi kabla ya ndege kuondoka

Ndege hiyo ilitarajiwa kusafiri kutoka uwanja wa ndege wa Calgary Canada kuelekea nchini Mexico Polisi huko Canada wamemkamata rubani mmoja aliyepatikana ,ndani ya ndege ya abiria kwenye chumba cha marubani akiwa amelewa chakari kwa mujibu wa vipimo alivyofanyiwa. Rubani huyo alikuwa amepangiwa kuendesha ndege hiyo kwa safari ya kutoka uwanja wa ndege wa Calgary Canada hadi nchini Mexico ndipo lakini wafanyikazi wenzake wakamuona hakuwa...

Aliyeweka nyama ya nguruwe msikitini afariki

Kevin aliweka vipande vya nyama ya nguruwe katika mlango wa msikiti wa Jamia huko Totterdown Mtu aliyeweka nyama ya nguruwe katika mlango wa msikiti nchini Uingereza amefariki akihudumia kifungo cha miezi 12 jela. Kevin Crehan alihukumiwa kifungo hicho katika mahakama ya Bristol Crown mnamo mwezi Julai kwa kuchochea machafuko ya uma. Vipande vya nyama ya nguruwe viliwekwa katika mlango wa msikiti wa Jamia huko Totterdown. Msemaji ...

Watu 39 wauawa wakikaribisha mwaka mpya Uturuki

Mshambuliaji aliyetekeleza mashambulio hayo alitoroka na hajakamatwa hadi kufikia sasa Takriban watu 39 wakiwemo wageni 15 wanahofiwa kuuawa katika shambulio la klabu ya burudani mjini Istanbul Uturuki, kulingana na waziri wa maswala ya ndani nchini humo. Mtu aliyekuwa amejihami kwa bunduki aliwafyatulia risasi watu waliokuwa wakijiburudisha katika mkahawa huo wa Reina saa saba usiku wakati ambapo watu walikuwa wakisherehekea...