Thursday, December 22, 2016

Roboti inayoweza kushiriki ngono kutengezwa

Roboti inayoweza kushiriki ngono na binadamu huenda ikazinduliwa mwaka ujao Je ungependelea kushiriki ngono na roboti? ungefunga ndoa na roboti? na Je roboti anaweza kuwa na haki ya kupinga ndoa hiyo? Haya ni baadhi ya maswala machache yanayoulizwa katika mkutano wa pili wa kuwa na mpenzi wa roboti mbali na kushiriki naye ngono katika chuo kikuu cha Goldsmith mjini London baada ya serikali ya Malaysia ambayo ndio iliokuwa...

Uwezo wa wanawake kupata mimba washuka Tanzania

Mji wa Dar es Salaam nchini Tanzania Viwango vya wanawake kuweza kupata mimba nchini Tanzania vimepungua hadi 5.2 kwa kila mwanamke nchini Tanzania mwaka 2015/2016 kutoka 6.2 kwa kila mwanamke miaka ya 1991/92, kulingana na utafiti wa afya nchini humo Kulingana na gazeti la The Citizen nchini Tanzania,utafiti huo uliofanywa na kutolewa na Afisi ya kitaifa ya Takwimu nchini humo NBS wiki iliopita unaonyesha kushuka...

Ujerumani wamtafuta kijana wa miaka 24

Mshukiwa wa shambulio la kigaidi huko nchiniUjerumani Polisi nchini Ujerumani wana mtafuta kijana wa miaka 24, Anis Amri raia wa Tunia kwa tuhuma za kuhusishwa na shambulio la lori katika soko la Christmas mjini Berlin nchini Ujeruman,ambapo watu 20 waliuawa. Anis ametajwa na vyombo vya usalama nchini Ujeruman kuwa ni mmoja wa watu hatari na anaye daiwa...

Kampuni ya Nokia yaishtaki Apple

Kesi hiyo ya Nokia imewasilishwa katika mahakama tatu nchini Ujerumani na Texas. Kampuni ya Nokia kutoka nchini Finland imesema kuwa inaishtaki kampuni ya Apple kwa kukiuka haki 32 za kiteknolojia. Kesi hiyo ya Nokia imewasilishwa katika mahakama tatu nchini Ujerumani na Texas. Madai hayo yanashirikisha matangazo, matumizi ya Interface, programu ,antena, chipu na alama za siri za vide...

Mkosoaji wa China ateuliwa kuongoza bodi ya biashara US

Rais mteule wa Marekani Donald Trump, amemtaja mkosoaji mkubwa wa biashara za Kichina Peter Navarro kuwa kiongozi mkuu wa baraza jipya la kibiashara katika Ikulu ya White Hous...

Tuesday, December 20, 2016

Marekani: Wajumbe waidhinisha ushindi wa Donald Trump

Wajumbe wa Jopo la Kuamua Mshindi wa Urais nchini Marekani wamemuidhinisha Donald Trump kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais uliofanyika Novemba. Hii ni licha ya juhudi za dakika za mwisho za kutaka kumzuia kuingia ikulu ya White...

Haikuwa matarajio ila Shule ya Ujerumani yapiga marufuku sherehe za Krismasi

Shule ya UJerumani nchini Uturuki Ripoti za vyombo vya habari kwamba shule moja ya Ujerumani nchini Uturuki imepiga marufuku sherehe za Krismasi imezua hisia kali nchini Ujerumani licha ya mamlaka ya shule hiyo kukana hatua hiyo. Kulingana na ripoti, wafanyikazi katika shule hiyo ya Lisesi iliopo mjini Istanbul waliambiwa kwamba tamaduni za Krisimasi na nyimbo za Carol hazitaruhusiwa tena. Wajumbe walitaja uamuzi huo...

Watu 3 wafariki katika maandamano DR Congo

Waandamanaji watatu wameuawa na wanajeshi katika mji mkuu wa DR Congo Kinshasa ,kulingana na mtandao wa polico.cd nchini humo. Watu wengine watano walijeruhiwa, wawili vibaya baada ya kupigwa risasi wakiwa karibu na maafisa wa kikosi cha Republican Guard katika mji wa N'djili mojawapo...

Monday, December 19, 2016

Trump na Clinton: Wajumbe kuamua mshindi wa urais Marekani

Bw. Donald Trump Wajumbe wa Jopo la Kumchagua Rais nchini Marekani wataanza utaratibu wa kuthibitisha matokeo ya uchaguzi wa urais nchini humo leo. Katika uchaguzi wa awali, mshindi wa kura nyingi kawaida alikuwa ndiye anapata kura nyingi za wajumbe, na hatua ya kumuidhinisha ilikuwa tu ya kutimiza wajibu. Lakini wakati huu, rais mteule Donald Trump wa chama cha Republican alishinda...

Tanzania: Waziri mkuu Majaliwa aunda tume kuchunguza hatima ya faru John

Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa amesema serikali imeunda tume kuchunguza taarifa inayoelezea utaratibu uliotumika kumhamisha faru John kutoka Hifadhi ya Ngorongoro kwenda Sasakwa Black Rhino Sanctuary iliyoko kwenye Hifadhi ya Grumeti Serengeti. Tume hiyo pia itatafuta kaburi la faru huyo ambaye inadaiwa alifariki. Amesema timu hiyo ya wataalamu tayari imeshafika Sasakwa VIP Grumet kwa ajili ya kutafuta kaburi na kuchukua vinasaba...

Hofu yatanda DRC CONGO kuelekea ukingoni mwa muhula wa Kabila

Rais Kabila ameongoza tangu mwaka 2001 Mzozo wa kisiasa unaendelea kutokota nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo huku muhula wa Rais Joseph Kabila ukifikia kikomo leo, kwa mujibu wa katiba. Mazungumzo ya kutafuta suluhu kati ya serikali na upinzani yaliahirishwa wiki iliyopita baada ya kukosekana kwa mwafaka. Mazungumzo hayo yanayoongozwa na maaskofu wa kanisa Katoliki yanatarajiwa kurejelewa Desemba 21. Kuna wasiwasi kwamba huenda...

Friday, December 9, 2016

Tunda Man-Debe tupu.New new

Kutoka kwa Tunda Man, Ngoma kali na mpya... Download h...